Alisema Bifwoli, mwanasiasa shetani
Alinena Wakoli, mwanasiaa mtani
Hukata makali, wakadai si vitani
Huzika wakali, kuondoa mitani
Vigeugeu wanasiasa, mipango tumbitumbi
Hudai sina sasa, ahadi kuteremshia ukumbi
Kwa misemo na visa, huinua nyingi vumbi
waitwe wa kisasa, wa zama huwa pimbi
Hutiumbuiza ikibidi, kuchochea upendo
Na pingamizi ikizidi, Fujo kwa si tendo
Wepesi wa ukaidi, hata kama ni uvundo
Ikiwazidi baridi, humtembelea Loliondo
Wananchi mna kazi, kujasusi na kuchagua
Sipumbazwe na vazi, humsetiri mchagua
Weka kwa makavazi, matendo ukikagua
Changanua yao makazi, na kwao kubagua
This poem has not been translated into any other language yet.
I would like to translate this poem