Bado Natamba Poem by priscah Mutswenje

Bado Natamba

Lenga mishale mwana, lenga tena mikali
Sije kuchoka mwana, kwayo yako makali
Silaha ya kufana, iwe kwako halali
Fuma sijakukana, fuma ilo mikali
Bado mie natamba, natamba nayo hali


Sio kwayo maneno, bali hata matendo
Kukwepa konokono, huuchuja vishindo
na mwema msono, hudhihaki mgando
ushindi ndilo neno, sipendi magendo
Bado mie natamba, natamba kwalo pendo


Kata kwa mtazamo, sitizame vya kando
Lenga kwacho kikomo, situpe pale kando
tumia huo mdomo, silaha iso pindo
Tupa na yaliyomo, sibakize la nondo
Bado mie natamba, natamba kimatendo



Kereketwa sifiche, tema kilo kooni
Maumbile ka cheche, sizime jioni
Rabana si mchache, huzisafisha mboni
kwa yote jikumbuche, kani'mba si shetani
Bado mie natamba, natamba upeoni

Bado Natamba
COMMENTS OF THE POEM
READ THIS POEM IN OTHER LANGUAGES
Close
Error Success